WELCOME NOTE

WELCOME NOTE

PICHA

PICHA

TANGAZO

Monday, September 24, 2012

VIELELEZO NA TEKNOLOJIA KWA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA


                   2.1 Vielezo na teknolojia kwa kufundishia na kujifunzia
                   2.2 Upatikanaji wa vielelezo na teknolojia                    
 
DHANA NA MAANA YA VIELELEZO NA TEKNOLOJIA KWA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA

Ni jumla ya zana au vifaa ikiwa ni asilia au vya kisasa vinavyoweza kutumiwa na mwalimu katika ufundishaji na kumsaidia kufundisha mada husika kwa ufanisi zaidi na mwanafunzi kuelewa mada hiyo kwa urahisi.
Mfano tufe,matunda,komputa,redio,projecta,vifani mbalimbali nk.
 
 SIFA ZA VIELELEZO NA TEKNOLOJIA KWA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA
i.                  Viwe sahihi katika muundo wake na kwa matumizi. Hii ina maana iwe na mjengo uliorahisi kuonekana, kupangwa na kupanguliwa
ii.         Viwe na ukubwa unaofaa. Hii ina maana zana iwe na ukubwa wa kati, kama ni chombo cha sauti, pia kiwe na sauti ya kati
iii.        Viwe na mvuto,ili kuvuta usikivu kwa walengwa.
iv.        Vishabihiane na ujumbe uliokusudiwa
v.         Vizingatie umri na uelewa wa walengwa
vi.        Viwe imara na vya kudumu
vii.       Visiwe na uwezo wa kupotosha dhana iliyokusudiwa
viii.      Viendane na mazingira halisi ya watoto
ix.        Vihamishike/viwe rahisi kubebeka.
NJIA ZA UPATIKANAJI WA VIELELEZO NA TEKNOLOJIA KWA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA 
Vielelezo vya kufundishia na kujifunzia vinaweza kupatikana katika njia kuu zifuatazo:
                                                                                i.            Kununuliwa.Mfano: Komputa,magazeti,redio,tepurekoda,projekta nk
                                                                               ii.            Kuazima.Mfano:-Kompyuta,projekta nk.
                                                                             iii.            Kuchukua/kutayarishwa kutoka mahali vilipohifadhiwa
                                                                             iv.            Kutengenezwa/kufaraguliwa,kama vile:-vifani vya viumbe hai,maumbo yenye ukumbi kama vile mche duara,mche mstatili,tufe nk.

No comments:

Post a Comment