WELCOME NOTE

WELCOME NOTE

PICHA

PICHA

TANGAZO

Tuesday, April 16, 2013

VIELELEZO NA TEKNOLOJIA KWA WENYE MAHITAJI MAALUMU


Mtoto wenye mahitaji maalumu:- Ni yule ambaye ama ana uwezo mkubwa kuliko wanafunzi wote wa kawaida au uwezo wake wa kujifunza na kuelewa ni mdogo sana au ana dosari katika maumbile yake. Mwalimu ataweza kutambua mtoto mwenye mahitaji maalumu kwa kuona kuwa matendo ni tofauti na watoto wengine. Hivyo basi mwalimu lazima awe na upeo na saikolojia kubwa ya kumwezesha kuwatambua watoto wenye mahitaji maalumu katika darasa lake.
Mfano wa  watoto wenye mahitaji maalumu ni:-
          Watoto wenye mtindio wa ubongo (taahira)
          Wasiiona (vipofu)
      Wasiosikia (viziwi)
          Wasiosema (bubu)
          Walemavu wa viungo vya mwili (vilema)
      Watoto wenye vipaji maalumu

(a) KUNDI LA WASIOONA
Kundi hili hujumuisha watoto wenye uoni hafifu ambao wanaweza kutumia vielelezo vya watu wa kawaida
Mwalimu anapaswa kuwawekea watoto wa namna hii karibu na ubao, kama utatumia michoro, picha sanjari na maandishi, yanalazimika yawe ni yenye kuonekana au maandishi yawe yaliyokuzwa.
Aina ya pili ya wasioona ni wale kusikia, kugusa, kunusa au kuonja. Hivyo basi vielelezo vifuatavyo vinaweza kutumika:-
  • Vitu halisi (kugusa, kuonja na kunusa)
  • Vinasa sauti/ tepurekoda (vielelezo na teknolojia masikizi).
  • Maandishi ya nukta nundu/ maandishi ya wasioona

(b) KUNDI LA WASIOSIKIA
Watu wa namna hii wamegawanyika katika makundi mawili. Wenye uwezo mdogo wa kusikia na wasiosikia kabisa. Wenye mdogo wa kusikia mwalimu anapaswa kuweka mbele ya darasa na kwa wale wasiosikia kabisa vielelezo na teknolojia vifuatavyo vinaweza kutumika:-
  • Vielelezo na teknolojiamaono (Picha, chati,  n. k)
  • Vitu halisi (wataona, watagusa na kuonja)
  • Lugha ya alama kwa wasiosikia
  • Kufuatisha mdomo (lips reading)

© KUNDI LA WASIOSEMA WALA KUSIKIA
Watu ambao hawana uwezo wa kusema wala kusikia, mwalimu anashauriwa kutumia vielelezo vifuatavyo:-
  • Lugha ya ishara
  • Vitu halisi kama vile miti, matunda, wanyama  n.k.
  • Picha mbalimbali Mfano, za wanyama, watu, mimea  n.k.

TANBIHI:- Watu kama wenye vipaji maalumu, walemavu wa miguu na wenye mtindio wa ubongo, Vilelelezo vinavyoweza kutumika kwa watu hawa vitawiana

No comments:

Post a Comment